Wednesday, December 24, 2014

IVORY COAST WAGOMEA BAJETI KIDUCHU WALIYOPEWA NA SERIKALI KWA AJILI YA AFCON.

SHIRIKISHO la Soka la Ivory Coast-FIF limegomea bajeti kiduchu waliyopewa na serikali ya nchi hiyo kwa ajili ushiriki wa timu ya taifa, katika michuano ya Mataifa ya Afrika-Afcon mwakani. Serikali ya nchi hiyo imekubali kutoa dola 575,805 kwa ajili ya timu hiyo itakayokwenda kushiriki fainali hizo zinazotarajiwa kuanza kutimua vumbi kuanzia Januari 17 hadi Februari 8 huko Guinea ya Ikweta. Pamoja na hayo, makamu wa rais w FIF, Sory Diabate amewaambia wana habari kuwa hawataweza kwenda kushiriki michuano hiyo kwa kiasi hicho cha fedha kwani walishawsilisha bajeti yao kwa ufafanuzi mzuri. Ivory Coast walikuwa wakitarajiwa kuanza mazoezi yao chini ya kocha Herve Renard huko Abu Dhabi, Januari 5 mwakani. Timu hiyo imepangwa katika kundi D sambamba na timu za Mali, Cameroon na Guinea.

No comments:

Post a Comment