Thursday, January 29, 2015

AFCON 2015: YAYA TOURE AZUSHA HOFU KUTOKANA NA MAJERUHI.

KIUNGO wa Ivory Coast Yaya Toure amezusha hofu kuhusiana na afya yake baada ya kulazimika kutolewa nje katika dakika za mwisho kwenye mchezo wa dhidi ya Cameroon. Kiungo huyo wa Manchester City alitolewa nje baada ya kukanyagwa na Stephane M’Bia lakini amesisitiza baada ya mchezo huo kuwa uwepo wake katika mchezo wa robo fainali dhidi ya Algeria hauna mashaka yeyote. Toure amesema hakuna tatizo lolote kubwa la kutisha hivyo kuwaondoa hofu mashabiki wao ambao tayari waliingiwa woga wa kumkosa shujaa wao huyo katika mchezo unaofuata. Katika mchezo huo bao pekee la Ivory Coast lilifungwa na Max Gradel katika dakika ya 36 ya kipindi cha kwanza na kuipa uongozi wa kundi D.

No comments:

Post a Comment