Thursday, January 29, 2015

AFCON 2015: KOCHA WA IVORY COAST ADAI NDIO KWANZA KIKOSI CHEK KIMEANZA AFCON.

KOCHA wa timu ya taifa ya Ivory Coast, Herve Renard amesema michuano ya Mataifa ya Afrika sasa ndio inaanza kwa timu yake baada ya kuichapa Cameroon kwa bao 1-0 na kumaliza vinara wa kundi D. Ivory Coast sasa wanakabiliwa na kibarua kizito mbele ya Algeria wakati watakapokwaana katika hatua ya robo fainali Jumapili hii. Renard amesema kama huwezi kupenya mbele ya timu kama Cameroon au Senegal lazima watu wakunyooshee vidole kuhusiana na uwezo wake. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa ukiwa na timu kama Ivory Coast mashindano huwa yanaanzia robo fainali kwasababu ukitoka mapema utakuwa umeshindwa. Renard amesema hatua hiyo itakuwa ngumu kwani kila timu inataka kufika fainali na wamebakisha hatua tatu pekee kulifikia taji la michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment