Thursday, January 29, 2015

ARSENAL YAMSAJILI RASMI PAULISTA KWA EURO MILIONI 15.

KLABU ya Arsenal imemsajili rasmi beki wa Villarreal Gabriel Paulista kwa kitita cha euro milioni 15 huku wakimtoa mshambuliaji Joel Campbell kujiunga na timu hiyo kwa mkopo mpaka mwishoni mwa msimu. Beki huyo wa kimataifa wa Brazil mwenye umri wa miaka 24 alikuwa sehemu muhimu ya kikosi cha Villarreal msimu huu na anaweza kupangwa katika mchezo wa Jumapili hii dhidi ya Aston Villa. Akihojiwa Paulista amesema alifanya mazungumzo na familia yake na kuwaambia kuwa ilikuwa ni ndoto zake kucheza katika Ligi Kuu hivyo mashabiki wa Arsenal wategemee mtu ambaye atajituma kadri ya uwezo wake ili kuisadia timu kushinda vitu muhimu. Arsenal walipewa kibali cha kufanyia kazi cha Paulista Jumatatu pamoja na ukweli kuwa nyota huyo hajawahi kuitumikia timu yake ya taifa na pia hatoki katika umoja wan chi za Ulaya. Paulista alijiunga na Villarreal akitokea klabu ya Vitoria ya nchini kwao Brazil mwaka 2013.

No comments:

Post a Comment