Thursday, January 29, 2015

TETESI ZA USAJILI ULAYA: MADRID WAPANGA KUCHUKUA DE GEA BURE KUTOKA MAN UNITED, PSG WAMTAKA ADEBAYOR KWA MKOPO.

KATIKA habari za tetesi za usajili klabu ya Real Madrid imepanga kumsajili golikipa wa Manchester United David De Gea mwenye umri wa miaka 24 wakati mkataba wake utakapoisha katika kipindi cha miezi 18 ijayo ili waweze kumchukua kama mchezaji huru. Klabu ya Paris Saint Germain imefanya mazungumzo na Tottenham Hotspurs kwa ajili ya kumsajili mshambuliaji wao Emmanuel Adebayor mwenye umri wa miaka 30 kwa mkopo mpaka mwishoni mwa msimu. Klabu ya Swansea City wanafikiria kujaribu kumsajili mshambuliaji wa Blackburn Ridy Gestede mwenye umri wa miaka 26 lakini mpaka sasa hakuna klabu yeyote iliyofikia dau la paundi milioni sita liliwekwa na timu hiyo ya daraja la kwanza. Meneja wa Liverpool Brendan Rodgers anafikiria kuwasajili viungo wa klabu ya Hannover Lars Stindl mwenye umri wa miaka 26 na Leonardo Bittencourt mwenye umri wa miaka 21 katika kipindi cha usajili wa kiangazi. Rodgers pia anajiandaa kutoa kitita cha paundi milioni 29 ili kuzizidi maarifa Paris Saint-Germain, Real Madrid na Juventus kwa ajili ya kiungo mwenye umri wa miaka 17 Ruben Neves ambaye anajulikana kama Sergio Busquets mpya akiwa katika klabu yake ya Porto. Wakala wa mshambuliaji wa Porto Jackson Martinez mwenye umri wa miaka 28 amesema mteja alikataa uwezekano wa kwenda Tottenham Hotspurs, Liverpool na Everton ili aweze kupata nafasi ya kucheza Serie A. Klabu ya Aston Villa imeanza tena mazungumzo ya kutaka kumsajili winga wa Manchester City Scott Sinclair mwenye umri wa miaka 25, ikiwa imepita siku chake baada ya kuonekana kama dili hilo halitawezekana.

No comments:

Post a Comment