Friday, January 30, 2015

COSTA AFUNGIWA MECHI TATU KWA KOSA LA KUMKANYAGA CAN WA LIVERPOOL.

MSHAMBULIAJI wa Chelsea, Diego Costa amefungiwa mechi tatu kwa kosa la kumkanyaga kwa makusudi mchezaji wa Liverpool Emre Can. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 26 anatarajiwa kuukosa mchezo wa Ligi Kuu kati ya timu yake na Manchester City utakaochezwa Stamford Bridge kesho pamoja na mechi dhidi ya Aston Villa na Everton. Chama cha Soka cha Uingereza-FA kilimtwanga adhabu hiyo ambayo Costa aliipinga kuhusiana na tukio lake alilofanya katika dakika ya 12 ya mchezo wa nusu fainali ya mkondo ya pili wa Kombe la Ligi uliofanyika Jumanne iliyopita. Costa aliyesajiliwa kwa kitita cha paundi milioni 32, ameshafunga mabao 17 katika mechi 19 za Ligi Kuu alizocheza simu huu. Tukio hilo halikuonwa na waamuzi lakini lilinaswa katika picha video.

No comments:

Post a Comment