Friday, January 30, 2015

LIVERPOOL YAPANIA KUMCHUKUA DANNY INGS KABLA YA KUFUNGWA KWA USAJILI WA DIRISHA DOGO.

KLABU ya Liverpool inatarajia kumsajili mshambuliaji wa Burnley Danny Ings kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili mdogo Jumatatu ijayo. Meneja wa Liverpool Brendan Rodgers yuko tayari kumchukua kwa mkopo nyota huyo mwenye umri wa miaka 22 kwa msimu uliobakia ili aweze kumalisha dili hilo. Ings ambaye anamalizia mkataba wake miezi sita uliobakia Burnley pia amekuwa akiwindwa na vilabu vya Tottenham Hotspurs na Real Sociedad. Hata hivyo, Burnley wanataka kuendelea kubakia na nyota huyo mpaka mkataba wake utakapomalizika mwishoni mwa msimu. Liverpool bado watatakiwa kulipa ada kama watamsajili Ings mwishoni mwa mkataba wake kutokana na kuwa chini ya umri w amiaka 24.

No comments:

Post a Comment