Friday, January 30, 2015

CHELSEA IKO KATIKA HATUA ZA MWISHO KUMNASA MCOLMBIA CUADRADO.

KLABU ya Chelsea iko katika hatua za mwisho kukamilisha dili la paundi milioni 23.3 kwa ajili ya usajili wa winga wa Fiorentina Juan Cuadrado mwenye umri wa miaka 26. Nyota huyo wa kimataifa wa Colombia tayari ameshafikia makubaliano kuhusu mambo yake binafsi na vinara hao wa Ligi Kuu na sasa klabu ziko katika hatua za mwisho kukamilisha uhamisho huo. Inakadiriwa kuwa Chelsea watatoa kitita cha paundi milioni 26.8 kwa ajili ya winga huyo kiasi ambacho ndio kilichowekwa na klabu yake hiyo ya Italia. Mohamed Salah mwenye umri wa miaka 22 anaweza kwenda kwa mkopo Fiorentina ikiwa ni sehemu ya kukamilisha dili hilo. Hata hivyo, winga huyo wa kimataifa wa Misri bado hajaamua kama anataka kwenda kuchheza Serie A au la.

No comments:

Post a Comment