Friday, January 30, 2015

MICHUANO YA AFCON YAFIKIA PATAMU WIKIENDI HII.

MICHUANO ya Mataifa ya Afrika-Afcon inaingia katika robo fainali ya mwishoni mwa wiki hii baada ya kumalizika kwa hatua makundi ambayo imetoa timu nane. Timu zilizotinga hatua hiyo ni pamoja na wenyeji Guinea ya Ikweta na Congo Brazzaville zilizofuzu kutoka kundi A, Tunisia na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo-DRC zilizofuzu kutoka kundi B huku Algeria na Coast na Ghana zenyewe zikitoka kundi C. Ivory Coast wenyewe walifuzu kutoka kundi D sambamba na Guinea ambao wao walifuzu kwa njia ya bahati nasibu baada ya kulingana alama na Mali. Kesho katika Uwanja wa Bata, wenyeji Guinea ya Ikweta itachuana na timu ngumu na wakongwe wa michuano hiyo Tunisia baada ya kumalizika kwa mchezo wa kwanza utakaowakutanisha majirani Congo Brazzaville na DRC. Jumapili vinara wanaopewa nafasi ya kutwaa taji hilo Algeria na Ivory Coast watakwaana huko Malabo kugombea nafasi ya kuingia nusu fainali, mchezo ambao utatanguliwa na Ghana ikichuana na Guinea.

No comments:

Post a Comment