Friday, January 30, 2015

MILAN YAMCHUKUA DESTRO KUTOKA KWA MAHASIMU WAO AS ROMA.

KLABU ya AC Milan imetangaza kumsajili kwa mkopo mshambuliaji nyota wa kimataifa wa wa Italia Mattia Destro kutoka kwa mahasimu wao wa Serie A AS Roma. Nyota huyo alifaulu vipimo vyake vya afya leo huku akitarajiwa kupewa mkataba wa moja kwa moja utakaoigharimu Milan euro milioni 16. Milan iko katika mchakato wa kuimarisha kikosi chake kufuatia kusuasua katika nusu ya kwanza ya msimu. Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 23 anarejea katika jiji la Milan akiwa mchezaji kamili baada ya kuanza soka lake katika shule ya vpaji ya Inter huku pia akiwa amewahi kuvaa jezi za Genoa na Siena kabla ya kujiunga na Roma Julai mwaka 2012. Toka atue Roma amefunga mabao 24 katika mechi 57 alizocheza lakini alishindwa kabisa kupata namba katika kikosi cha kwanza msimu huu hivyo kuruhusiwa kuondoka.

No comments:

Post a Comment