Friday, January 30, 2015

PIQUE NA SHAKIRA WAPATA MTOTO WA PILI.

BEKI wa Barcelona, Gerard Pique na mwanamuzi nyota Shakira wamefanikiwa kupata mtoto wao wa pili aliyezaliwa jana usiku. Shakira alijifungua mtoto wa kiume bila matatizo yeyote katika hospitali ya Quiron Tecknon iliyopo jijini Barcelona. Pique mwenye umri wa miaka 27 na mwanamuziki huyo wa Pop kutoka Colombia mwenye umri wa miaka 27, walitoa taarifa hizo muda mfupi kabla ya usiku wa manane. Jina la mtoto ambaye amezaliwa miaka miwili baada ya wawili hao kupata mtoto wao wa kwanza aitwaye Milan bado halijawekwa wazi. Wawili hao wamekuwa pamoja toka mwaka 2010 walipokutana katika michuano ya Kombe la Dunia iliyofanyika nchini Afrika Kusini.

No comments:

Post a Comment