Friday, January 30, 2015

LEVANTE YAMCHUKUA MKONGWE UCHE.

KLABU ya Levante imetangaza kumsajili kiungo wa ushambuliaji wa kimataifa wa Nigeria Kalu Uche. Uche mwenye umri wa miaka 32 ambaye pia anaweza kucheza nafasi ya ushambuliaji amejiunga na klabu hiyo kwa mkataba wa miezi sita akiwa mchezaji huru. Nyota huyo ataweza kuongezwa mkataba mwingine kulingana na jinsi msimu utakavyokwenda kwa klabu hiyo ambayo inapambana isishuke daraja. Uche aliondoka katika klabu ya Al Rayyan ya Qatar na kurejea nchini Hispania kwa mara ya kwanza baada ya kupita miaka miwili. Levante imechukua kiungo huyo ili kuimrisha safu yake ya ushambuliaji ambayo msimu huu imefanikiwa kufunga mabao 13 pekee katika mechi 16 walizocheza. Kabla ya kutimkia Qatar Uche aliwahi kuzichezea klabu za Almeria na Espanyol.

No comments:

Post a Comment