Friday, January 30, 2015

ETO'O AAHIDI KUISAIDIA SAMPDORIA KUSHIRIKI LIGI YA MABINGWA ULAYA.

MSHAMBULIAJI wa zamani wa kimataifa wa Cameroon, Samuel Eto’o ameeleza matamanio yake ya kuisaidia Sampdoria kufuzu katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kutambulishwa mbele ya wanahabari jana. Nyota huyo amesaini mkataba wa miaka miwili na nusu katika klabu hiyo ya Serie A na kumaliza kipindi chake kifupi alichokaa Everton. Toka alipoichukua klabu hiyo mwaka jana, mmiliki Massimo Ferrero amekuwa akielezea matamanio yake ya kuinoa Sampdoria ikifuzu michuano hiyo na Eto’o anafikiri ni malengo yanayowezekana. Eto’o mwenye umri wa miaka 33, amesema ameonyesha kwamba kwa kufanya kazi kwa bidii na kufuata ndoto zake kila kitu kinawezekana kwani amefanikiwa na kuwa mmoja kati ya wachezaji wakubwa kabisa duniani. Nyota huyo aliendelea kudai kuwa kutokana na hilo raia wa klabu hiyo ana haki ya kuwa na ndoto na kutimiza ndoto zake.

No comments:

Post a Comment