Friday, January 30, 2015

URENO YAMUUNGA MKONO FIGO KWA UAMUZI WAKE.

UAMUZI wa Luis Figo kuingia katika kinyang’anyiro cha kugombea urais wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA imepokewa vyema nchini kwake Ureno pamoja na kukabiliwa na kibarua kigumu mbele ya rais wa sasa Sepp Blatter katika uchaguzi utakaofanyika Mei mwaka huu. Figo mwenye umri wa miaka 42 ambaye amewahi kushinda tuzo ya mchezaji bora wa dunia na mmoja kati ya wachezaji bora katika kipindi chake akiwa Real Madrid na Barcelona alitangaza nia yake hiyo Jumatano iliyopita baada ya kukamilisha vigezo vilivyohitajika. Muda wa mwisho wa kutuma maombi utakuwa leo usiku huku huku Figo akiwa sambamba na wagombea wengine wasiomtaka Blatter na kutangaza nia akiwemo Prince Ali Bin Al-Hussein kutoka Jordan, Michael van Praag kutoka Uholanzi na Jerome Champagne na David Ginola wote kutoka Ufaransa. Rais wa Shirikisho la Soka la Ureno-FPF, Fernando Gomes amesema jana kuwa kujitokeza kwa FIGo kugombea nafasi hiyo ni heshima kubwa kwa soka la nchi hiyo hivyo watamuunga mkono mpaka mwisho wa safari yake. Waziri wa michezo wa Ureno Emidio Guerreiro pia alitangaza serikali kumuunga mkono kiungo huyo wa zamani ambaye ameliletea taifa hilo sifa kemkem.

No comments:

Post a Comment