Friday, January 30, 2015

WEST HAM YADAI KUFUATA TARATIBU ZOTE KWA KUMTUMIA SAKHO.

MENEJA wa West Ham United, Sam Allardyce hategemei Diafra Sakho kufungiwa kwa kuitumikia klabu hiyo baada ya kujitoa katika kikosi cha Senegal kilichoshiriki michuano ya Mataifa ya Afrika. Mshambuliaji huyo alishindwa kuwepo katika cha nchi hiyo kilichokuwa Guinea ya Ikweta kutokana na kusumbuliwa na matatizo ya mgongo. Hata hivyo, alitokea benchi na kuifungia West Ham bao la ushindi mwishoni mwa wiki katika mchezo wa Kombe la FAdhidi ya Bristol City huku nchi yake ikiwa bado inashiriki Afcon kwa wakati hu. Shirikisho la Soka Duniani-FIFA limethibitisha kupokea malamiko kutoka Shirikisho la Soka la Senegal kuhusiana na suala hilo. Hata hivyo, Allardyce amesema hana shaka kama nyota huyo atapewa adhabu yeyote kwani wamefuata sheria na taratibu zote zilizopo.

No comments:

Post a Comment