Wednesday, January 28, 2015

FIGO NAYE AJITOSA KINYANG'ANYIRO CHA URAIS FIFA.

NGULI wa soka wa Ureno, Luis Figo ametangaza uamuzi wake wa kugombea nafasi ya urais wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Mei mwaka huu. Figo amechukua uamuzi huo wa kugombea nafasi ya hiyo siku muda kabla ya muda wa mwisho wa kutuma maombi baada ya kukusanya vielelezo vyake vikiwemo vyama vitano vya soka vinayomuunga mkono. Akihojiwa na CNN, Figo amesema anajali mpira hivyo anachikiona sasa katika taswira ya FIFA hakubaliani nacho ndio maana ameamua kugombea nafasi hiyo ili kumng’oa rais wa sasa Sepp Blatter ambaye amepanga kugombea kwa kipindi cha tano. Figo aliendelea kudai kuwa kama utaitafuta FIFA katika mtandao jambo la kwanza litakalokuja ni kashfa mbalimbali zinazoiandama katika miaka ya karibuni jambo ambalo sio zuri kwa ukuaji wa soka. Figo amesema amezungumza na watu wengi muhimu katika soka, wachezaji, mameneja, marais wa mashirikisho na wote wanadhani kunatakiw akufanyka mabadiliko. Mshambuliaji huyo wa zamani wa vilabu vya Barcelona, Real Madrid na Inter Milan ameungana na Jerome Champagne, Prine Ali Bin Hussein, David Ginola na Michael van Praag ambao tayari wametangaza nia hiyo ya kupambana na Blatter.

No comments:

Post a Comment