Wednesday, January 28, 2015

MOURINHO ALIMWA FAINI KWA UTUKUTU.

MENEJA wa Chelsea, Jose Mourinho ametozwa faini ya paundi 25,000 kwa kauli yake aliyodai kuna kampeni za makusudi zinazofanywa na waamuzi kuidhoofisha timu yake. Mourinho alitoa kauli hiyo baada ya kikosi chake kukataliwa penati katika mchezo uliomalizika kwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Southampton Desemba 28 mwaka jana. Chama cha Soka cha Uingereza-FA kimemtoza faini kwa kauli hiyo ambayo inaweza kuleta mkanganyiko katika soka huku akionywa kutofanya kosa kama hilo katika siku za usoni. Mbali na hilo Mourinho pia alionywa kwa kauli yake aliyotoa kabla ya mchezo kati ya Chelsea na Stoke City Desemba 22 ambao walikuja kushinda kwa mabao 2-0.

No comments:

Post a Comment