Wednesday, January 28, 2015

TETESI ZA USAJILI ULAYA: MADRID WATAKA KUZIBA PENGO LA COENTRAO KWA KUMCHUKUA GAYA, LIVERPOOL YAKARIBIA KUMCHUKUA LAVEZZI, PARDEW AMTAKA ZAHA MOJA KWA MOJA.

KATIKA habari za tetesi za usajili klabu ya Real Madrid imedaiwa kutaka kuziba nafasi ya Fabio Coentrao na kuripotiwa kuwa wanajipanga kumuwinda chipukizi wa Valencia Jose Luis Gaya mwenye umri wa miaka 19. Kama Madrid watahitaji saini ya chipukizi huyo watalazimika kutoa kitita cha euro milioni 18 kilichowekwa na Valencia. Klabu ya Liverpool inakaribia kufikia makubaliano ya euro milioni 20 na Paris Saint Germain kwa ajili ya kumsajili Ezeguiel Lavezzi. Kiungo wa klabu ya Hannover Lars Stindl ameripotiwa kukaribia kukamisha usajili wake wa kujiunga na Schalke 04. Stindl mwenye umri wa miaka 26 anatarajiwa kuondoka Hannover katika majira ya kiangazi kwa kitita cha paundi milioni tatu kitakachotolewa na Schalke. Kiungo wa West Ham United Ravel Morrison anatarajiwa kukamilisha uhamisho wake kwenda klabu ya Lazio lakini klabu hiyo ilimzuia nyota huyo mwenye umri wa miaka 21 kusafiri kwenda jijini Rome jana kusaini mkataba wa awali. Gabriel Paulista anatarajiwa kuanza katika kikosi cha kwanza cha Arsenal haraka kufuatia kuwasili kwake kutoka Villarreal na anaweza kuwepo katika mchezo dhidi ya Aston Villa utakaochezwa Jumapili. Tetesi za Darren Fletcher kuondoka Manchester United zimezaa matunda baada ya sasa klabu za West Ham United, West Bromwich Albuon na Valencia kuonyesha nia ya kutaka kumsajili kiungo huyo mwenye umri wa miaka 30. Klabu ya Crystal Palace inataka kumsajili Wilfried Zaha kwa mkataba wa moja kwa moja huku kocha Alan Pardew akitaka kutanguliza kwanza kiasi cha paundi milioni tatu na baadae kumalizia paundi milioni tatu zilizobakia.

No comments:

Post a Comment