Monday, January 26, 2015

RATIBA YA FA: ARSENAL WAPANGWA NA WABABE WA CITY, MAN UNITED KUENDELEA KUPETA KAMA WAKISHINDA MECHI YAO YA MARUDIANO DHIDI YA CAMBRIDGE.

MABINGWA watetezi Arsenal wamepangwa na timu ya daraja ya kwanza la Middlesbrough katika mzunguko wa tano wa michuano ya Kombe la FA. Middlesbrough ambao waliing’oa Manchester City katika mzunguko wa nne wataifuata Arsenal katika uwanja wao wa Emirates mwishoni mwa wiki ya Februari 14 na 15 mwaka huu. Bradford City waliopo ligi daraja la pili wao wamezawadiwa kwa kuitoa Chelsea kwa kupewa mchezo wa nyumbani dhidi ya aidha Sunderland au Fulham. Mshindi katika mchezo kati ya Cambridge United na Manchester United anatarajiwa kukutana na aidha Preston au Sheffield United. Katika michezo mingine ya mzunguko wa tano Crystal Palace wao watakuwa wenyeji wa mshindi kati ya Liverpool au Bolton Wanderers wakati Aston Villa watakwaana na Leicester City na West Bromwich Albion wao watachuana na West Ham United.

No comments:

Post a Comment