Saturday, January 24, 2015

TETESI ZA USAJILI ULAYA: JUVENTUS KUMUUZA POGBA KWA EURO MILIONI 100 KIANGAZI, CHELSEA YAONGEZA DAU KWA COSTA.

KATIKA habari za tetesi za usajili klabu ya Juventus imepanga kumuachia Paul Pogba kama watapewa ofa ya paundi milioni 100 katika kipindi cha majira ya kiangazi. Klabu za Manchester City, United na Chelsea zinamfukuzia nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa kama ilivyo kwa klabu za Paris Saint-Germain na Bayern Munich. Chelsea wameongeza ofa yao kufikia euro milioni 25 kwa ajili ya kumsajili Douglas Costa huku wakijipanga pia na kumsajili Juan Cuadrado wa Fiorentina. Nyota hao wa Amerika Kusini wanategemewa kutua Stamford Bridge kuja kuziba nafasi ya za Andre Schurrle na Mohamed Salah ambao wanatarajiwa kuondoka katika kipindi hiki cha usajili wa Januari. Manchester United wameamua kumvalia njuga beki wa kulia wa Southampton Nathaniel Clyne ambapo wamemua kumtengea ofa ya kitita cha euro milioni 27. Meneja wa Queens Park Rangers, Harry Redknapp anajipanga kumfukuzia mshambuliaji wa Monaco Dimitar Berbatov katika kipindi hiki cha usajili wa Januari. Nyota huyo alimuambia Redknapp kuwa anataka kurejea katika Ligi Kuu huku akidaiwa kuigharimu QPR euro milioni 1.3 kama wakimchukua. Klabu za Manchester United na Arsenal zinapigana vikumbo katika kumfukuzia nyota wa klabu ya Dinamo Moscow Aleksandar Dragovic ambapo meneja Arsene Wenger ameamua kutuma maskauti wake kumuangalia katika mchezo wa kirafiki. Wenger anamchukulia mchezaji huyo kama karata yake ya pili kama akishindwa kumsajili Gabriel Paulista.

No comments:

Post a Comment