Friday, January 23, 2015

TETESI ZA USAJILI ULAYA: CHELSEA YAKUBALI KUIPA FIORENTINA PAUNDI MILIONI 23 KWA AJILI YA CUADRADO, MAN UNITED YAMVIZIA ALVES KIANGAZI.

KATIKA habari tetesi za usajili, klabu ya Chelsea hatimaye imefikia makubaliano na klabu ya Fiorentina kwa ajili ya kumsajili Juan Cuadrado kwa kitita cha paundi milioni 23. Chelsea sasa wameruhusiwa kuzungumza na nyota huyo wa kimataifa wa Colombia mwenye umri wa miaka 26 kwa ajili ya makubaliano binafsi wakati wakijipanga kumuuza Mohamed Salah. Arsenal wameingia katika kinyang’anyiro cha kumuwania kiungo wa Roma Radja Nainggolan lakini wanakabilwia na kibarua kizito kutoka na klabu za Manchester United na Chelsea nazo kumuwinda kiungo huyo anayekadiriwa kuwa na thamani ya paundi milioni 26. Manchester United wanazidisha kupata uhakika wa kumsajili Dani Alves kutoka Barcelona kwa uhamisho huru katika majira ya kiangazi. Kocha wa United Louis van Gaal amepania kumsajili beki huyo wa kulia na anamatumaini Victor Valdes anaweza kumshawishi mchezaji mwenzake wa zamani kuhamia Old Trafford. Kiungo Yann M’Vila amerejea katika klabu yake ya Rubin Kazan baada ya Inter Milan kuamua kutengua mkpo wa mchezaji huyo kufuatia kuonyesha kiwango kibovu. Liverpool nao wanajipanga kutoa ofa kwa ajili ya kumsajili mshambuliaji wa Southampton Jay Rodriguez kabla ya dirisha la usajili wa Januari halijafungwa. Winga huyo wa kimataifa wa Uingereza anatarajiwa kurejea uwanjani baada ya kupona majeruhi yaliyokuwa yakimsumbua wiki hii. Manchester United wanajipanga kufanya usajili wa wachezaji watatu wakubwa katika majira ya kiangazi ambapo kocha Louis Van Gaal amepanga kuwasajili kiungo wa Roma Kevin Strootman, beki wa Borussia Dortmund Mats Hummels na beki wa kulia wa Southampton Nathaniel Clyne.

No comments:

Post a Comment