Friday, January 23, 2015

MADRID YAMNASA LUCAS SILVA.

MAKAMU rais wa klabu ya Cruzeiro Marcio Rodriguez amedai kuwa uhamisho wa Lucas Silva kwenda Real Madrid umeshafikia hatua nzuri ya makubaliano. Kwa kipindi kirefu Madrid iliyo chini Carlo Ancelotti imekuwa ikimfukuzia kiungo huyo chipukizi mwenye umri wa miaka 21. Rodriguez amesema uhamisho wa Silva tayari umekamilika na kilichokuwa kikisubiriwa ni Madrid wenyewe kutangaza rasmi. Rodriguez aliendelea kudai kuwa hawata pata tabu kutafuta mbadala wake kwani kuna wachezaji wengi ambao wako tayari kupandishwa.

No comments:

Post a Comment