Friday, January 23, 2015

TER STEGEN AAPA KUPIGANIA NAMBA BARCELONA.

GOLIKIPA wa kimataifa wa Ujerumani Marc-Andre Ter Stegen amekiri kuwa hana furaha katika nafasi yake kama gilikipa namba mbili na amejipanga kuhakikisha anakuwa kinara wa klabu ya Barcelona. Golikipa huyo mwenye umri wa miaka 22 alijiunga na Barcelona akitokea Borussia Monchengladbach Mei mwaka jana lakini kocha Luis Enruque anamtegemea zaidi Claudio Bravo kama kipa namba moja. Hata hivyo, Ter Stegen bado anamatumaini kuwa ataweza kumzidi uwezo golikpa huyo wa kimataifa wa Chile wakati wowote katika msimu huu unaondelea. Akihojiwa Ter Stegen amesema anafurahia anavyoungwa na mkono na mashabiki na kazi anayofanya na wachezaji wenzake lakini hafurahishwi na kuwa kwake chaguo la pili.

No comments:

Post a Comment