Friday, January 23, 2015

RONALDO ANAWEZA KUITUMIKIA MADRID KWA MIAKA 10 ZAIDI - MENDES.

WAKALA wa mshambuliaji nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo amedai kuwa mteja wake huo bado ana miaka 10 zaidi ya kuendelea kuitumikia klabu hiyo. Nyota huyo wa kimataifa wa Ureno mapema mwezi huu alinyakuwa tuzo yake ya tatu ya Ballon d’Or ikiwa ni ya pili toka atue Santiago Bernabeu lakini hivi karibuni amekaririwa akidai kuwa anafikiria kuhamia nchini Brazil kabla ya kutundika daruga zake. Hata hivyo wakala huyo Jorge Mendes ana uhakika Ronaldo atamalizia soka lake akiwa Madrid huku akidai kuwa nyota huyo bado ana miaka 10 zaidi ya kucheza soka katika kiwango cha juu. Mendes amesema ana uhakika Ronaldo atastaafu akiwa Madrid na umri wa miaka 38 au 39 kwasababu bado ana miaka mingi ya kucheza soka. Mendes aliendelea kudai kuwa kikubwa kinachomfanya kuamini kwamba anaweza kufikia huko ni kutokana na jinsi anavyojiweka fiti mpaka kuwa mfano kwa wachezaji wenzake.

No comments:

Post a Comment