Thursday, January 22, 2015

TETESI ZA USAJILI ULAYA: CHELSEA YAMTENGEA PAUNDI MILIONI 40 WINGA WA FIORENTINA, UNITED NAO WAINGIA KATIKA MBIO ZA KUMUWANIA PAULISTA.

KATIKA habari za tetesi za usajili klabu ya Chelsea inaripotiwa kuanza mazungumzo na Fiorentina kwa ajili ya kumsajili winga wa kimataifa wa Colombia Juan Cuadrado mwenye umri wa miaka 26 katika kipindi hiki cha usajili. Vinara hao wa Ligi Kuu wanadaiwa kuongeza nguvu katika harakati zao za kumsajili winga huyo baada ya ofa yao ya paundi milioni 20.6 kukataliwa jana. Chelsea wanadaiwa kutaka kufidia gharama za Cuadrado kwa mauzo ya winga Mohamed Salah mwenye umri wa miaka 22 au mshambuliaji Andre Schurrle mwenye umri wa miaka 24. Schurrle anaripotiwa kujipanga kurejea katika klabu ya Wolfsburg ya nchini kwake Ujerumani. Mbali na hayo Chelsea pia inahusishwa na taarifa za kutenga kitita cha paundi milioni 40 kwa ajili ya kumuwania kiungo wa Juventus Paul Pogba mwenye umri wa miaka 21 ambaye aliondoka Manchester United mwaka 2012. Klabu ya Valencia nayo imejipanga kuizidi kete Liverpool kwa kusajili kiungo wa Manchester James Milner mwenye umri wa miaka 26. Arsenal wanatarajiwa kuchuana na Manchester United katika kuwania kumsajili beki wa kati wa Villarreal Gabriel Paulista ambaye anakadiriwa kuwa na thamani ya paundi milioni 16.

No comments:

Post a Comment