Wednesday, January 28, 2015

STOKE YAPATA PIGO, BAADA YA BOJAN KUTAKIWA KUKAA NJE YA UWANJA MSIMU WOTE ULIOBAKIA.

MSHAMBULIAJI wa Stoke City Bojan Krkic anatarajiwa kuukosa msimu mzima uliobakia baada ya kuumia goti katika mchezo wa Kombe la FA mzunguko wa nne dhidi ya Rochdale uliochezwa Jumatatu. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Hispania mwenye umri wa miaka 24 ndiye aliyefunga bao la kuongoza katika mchezo huo ambao Stoke waliibuka na ushindi wa mabao 4-1 lakini yeye alitolewa katika dakika ya 32 baada ya kuumia. Katika taarifa iliyotumwa katika mtandao wa klabu hiyo ilithibitisha taarifa hizo huku ikidai kuwa vipimo vinaonyesha kuwa nyota huyo alichanika msuli wa ndani ya goti lake la kushoto. Stoke walimsajili mshambuliaji huyo ambaye ameitwa mara moja kuitumikia Hispania, kutoka Barcelona kwa mkataba wa miaka minne Julai mwaka jana.

No comments:

Post a Comment