Wednesday, January 28, 2015

FABREGAS HATIHATI KUIKOSA CITY JUMAMOSI.

KUNA wasiwasi mkubwa wa kiungo wa Chelsea Cesc Fabregas kuukosa mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya mahasimu wao katika mbio za ubingwa Manchester City Jumamosi hii kutokana na majeruhi ya msuli wa paja yanayomsumbua. Fabregas alilazimika kutolewa katika mchezo wa Kombe la Ligi ambao Chelsea ilifanikiwa kushinda bao 1-0 dhidi ya Liverpool na kutinga hatua ya fainali. Meneja wa Chelsea Jose Mourinho amesema Fabregas alitoa taarifa ya kukazkwa msuli wake wa paja na kudai kuwa alikuwa hajaumia bado ila angeweza kuumia kama angeendelea kucheza. Mbali na Fabregas pia mabeki Filipe Luis na Branislav Ivanovic na wanahofiwa kuwa majeruhi na kuukosa mchezo huo muhimu. Chelsea ndio vinara wa ligi wakitofautiana kwa alama tano na City wanaoshika nafasi ya pili.

No comments:

Post a Comment