Wednesday, January 28, 2015

MESSI ADAI LEO KUFA NA KUPONA LAZIMA WAITANDIKE ATLETICO.

MSHAMBULIAJI wa Barcelona, Lionel Messi ameapa kufanya kila wawezalo kuifunga Atletico Madrid ili kujihakikishia nafasi ya kutinga nusu fainali ya Kombe la Mfalme. Timu hizo zinatarajiwa kukwaana katika Uwanja wa Vincente Calderon kwa ajili ya mechi ya robo fainali ya mkondo wa pili huku Barcelona wakiongoza kwa bao 1-0 walilopata katika mchezo wa mkondo wa kwanza uliofanyika katika Uwanja wa camp Nou. Messi aliandika katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa facebook kuwa ana hamu kubwa ya mchezo huo na kwamba yeye na wachezaji wenzake wamepania kufanya kila wawezalo kuhakikisha wanatinga hatua ya nusu fainali. Barcelona ilitinga hatua ya fainali ya michuano hiyo msimu uliopita lakini walijikuta wakichapwa na Real Madrid.

No comments:

Post a Comment