Thursday, January 1, 2015

SWANSEA YAKUBALI ADHABU YA SHELVEY.

KLABU ya Swansea City imekubali adhabu ya kiungo Jonjo Shelvey kufungiwa mechi nne baada ya kukutwa na hatia ya kumpiga kiwiko mchezaji wa Liverpool Emre Can. Shelvey alimtwanga kiwiko Can usoni wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ambao Swansea walitandikwa mabao 4-1 na Liverpool. Katika mchezo huo mwamuzi Andre Marriner hakuliona tukio hilo hivyo alimruhusu Shelvey mwenye umri wa miaka 22 kuendelea na mchezo. Katika taarifa yake iliyotumwa katika mtandao Swansea walithibitisha kukubali adhabu hiyo huku Chama cha Soka cha Uingereza-FA kikidai kuwa pamoja na kuwa tukio hilo halikuonwa na mwamuzi lakini picha za video ndio zilizothibitisha kutokea kwake.

No comments:

Post a Comment