Wednesday, December 31, 2014

KAPUNOVIC ATUA TAYARI KUINOA SIMBA.

HATIMAYE kocha mpya wa klabu ya Simba, Goran Kopunovic raia wa Serbia amewasili jijini Dar es Salaam leo asubuhi huku akitamba kuwa anaifahamu yanga vizuri. Akihojiwa na blog ya Bin Zubeiry, baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa, Dar es Salaam, kocha huyo kijana amesema mafurahi kuja kuinoa Simba kwani ni klabu kubwa na amepania kuiletea mafanikio. Kapunovic amesema anatarajia kukutana na uongozi wa Simba kwa mazungumzo na kusaini mkataba na baada ya hapo ataanza kazi rasmi. Akizungumzia kuhusu wapinzani wa jadi, Yanga SC, Kopunovic amesema kwamba anawajua vizuri na anafahamu kuhusu soka ya Tanzania kwa ujumla. Kapunovic anakuja baada ya kutimuliwa kwa kocha Patric Phiri kutoka Zambia kutokana na matokeo yasiyoridhisha ya timu hiyo kikiwemo kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Kagera Sugar.

No comments:

Post a Comment