Wednesday, December 31, 2014

CISSE AKUBALI YAISHE.

MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Newcastle United, Papiss Cisse amekubali kosa lake alilofanya katika mchezo wa Ligi Kuu kati ya timu yake dhidi ya Everton. Cisse ambaye amefunga mabao tisa msimu huu, alimpiga kiwiko beki Seamus Coleman katika mchezo huo wa Jumapili iliyopita na anatarajiwa kutumikia adhabu ya mechi tatu. Nyota huyo sasa atakosa mechi za ligi dhidi ya Burnley na vinara Chelsea na mchezo wa mzunguko wa tatu wa Kombe la FA dhidi ya Leicester City. Katika mchezo huo Newcastle walishinda kwa mabao 3-2 dhidi ya Everton.

No comments:

Post a Comment