Wednesday, December 31, 2014

NASRI AITISHA CHELSEA KUWA WAO WANAFUKUZA MWIZI KIMYA KIMYA.

KIUNGO wa klabu ya Manchester City Samiri Nasri amewaonya mahasimu wao Chelsea kuwa timu ina uzoefu wa kuwafukuzia katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu. Kikosi cha City kilicho chini Manuel Pellegrini kinashika nafasi ya pili mbele ya vinara Chelsea kwa tofauti ya alama tatu wakati wakijiandaa na mchezo dhidi ya Sunderland kesho. City walifanikiwa kushinda taji la ligi msimu uliopita pamoja na kuwa nyuma ya Arsenal na Liverpool kwa kipindi kirefu wakati wa kampeni hizo na Nasri anaamini kuwa uzoefu huo unawapa nafasi katiika mbio za ubingwa msimu huu. Akihojiwa Nasri amesema kila mmoja anakuwa imara na kadri umri wao unavyozidi kusonga mbele ndio uzoefu nao unaongezeka. Nasri aliendelea kudai kuwa wanajifunza mambo mengi katika timu hiyo kwani wameshapitia mambo mengi tofauti hivyo wanajua jinsi gani ya kukabiliana na changamoto.

No comments:

Post a Comment