Wednesday, December 31, 2014

RONALDO NI BORA LAKINI MESSI ANAKIPAJI CHA KIPEKEE - RAKITIC.

MCHEZAJI nyota wa kimataifa wa Croatia, Ivan Rakitic anadhani kuwa wakati Cristiano Ronaldo akiwa mchezaji bora, Lionel Messi ni mchezaji wa mwenye kipaji cha kipekee ambacho kinamfanya kuwa juu ya kila mchezaji katika sayari hii. Ronaldo na Messi wote wapo katika orodha ya kugombea tuzo ya Ballo, d’Or sambamba na golokipa wa kimataifa wa Ujerumani Manuel Neuer. Ronaldo amevunja rekodi ya ufungaji wakati akiisaidia Real Madrid kushinda taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya, Kombe la Klabu Bingwa ya Dunia na Kombe la Mfalme katika miezi 12 iliyopita. Kwa upande wa Neuer yeye ameisaidia Bayern Munich kushinda mataji mawili kabla ya kuwa sehemu muhimu katika kikosi cha Ujerumani kilichonyakuwa Kombe la Dunia mwaka huu nchini Brazil. Rakitic anafahamu vyema uwezo wa wawili hao ingawa hata hivyo anadai hajawahi kukutana na yeyote anayefikia kiwango cha Messi na anadhani anastahili kuchukua tuzo hiyo. Rakitic amesema kuna mmoja pekee ambaye yuko juu ya wote naye ni Messi halafu wengine ndio wanafuatia.

No comments:

Post a Comment