Wednesday, December 31, 2014

ODIMWINGIE KUPEWA MKATABA NA STOKE.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Nigeria, Peter Odemwingie anatarajiwa kupewa mkataba mpya na klabu ya Stoke City pamoja na kuwa nje ya uwanja kutokana na majeruhi. Odemwingie amekuwa nje toka Agosti akisumbuliwa na majeruhi ya goti lakini nyota huyo wa zamani wa West Bromwich Albion na Cardiff City anatarajia kumaliza mkataba wake na Stoke mwishoni mwa msimu huu. Hata hivyo kumekuwa na taarifa njema kwake kwani Stoke wanapanga kumuongeza mkataba wa mwaka mmoja zaidi pamoja na kufikisha umri wa miaka 34 msimu ujao. Meneja wa Stoke Mark Hughes amebainisha kuwa kila kitu sawa kwa Odemwingie pamoja na kuwa nje kwa kipindi kirefu msimu huu. Nyota huyo tayari ameanza mazoezi ya kukimbia nje na anakaribia kurejea katika afya yake ya kawaida.

No comments:

Post a Comment