Wednesday, December 31, 2014

BLANC KUTOA UAMUZI WA MWISHO KUHUSIANA NA SUALA LA CAVANI NA LAVEZZI.

MENEJA wa klabu ya Paris Saint-Germain-PSG Laurent Blanc amesema anasubiri ufafanuzi kabla ya kutoa uamuzi kuhusiana na mustakabali wa Edinson Cavani na Ezequiel Lavezzi. Hakuna mshambuliaji yeyote kati ya hao aliyesafiri na kikosi cha PSG karika ziara yao ya Morocco hivyo kuzidisha tetesi kuwa klabu hiyo inaweza kusikiliza ofa zitakazotolewa katika kipindi cha usajili mwezi ujao. Cavani amekuwa akihusishwa na tetesi za kwenda Arsenal, wakati Liverpool na Inter Milan wao wameripotiwa kumtaka Lavezzi. Hata hivyo, Blanc amesisitiza hakuna kilichoamuliwa mpaka wachezaji hao watakaporejea kwa ajili ya mazoezi Januari 2. Blanc amesema wanasubiri baadhi ya ufafanuzi kutoka kwao wakati watakapowasili ndipo watoe uamuzi wao kuhusiana na mustakabali wao.

No comments:

Post a Comment