Wednesday, December 31, 2014

BAADA YA KUHARIBU SHEREHE YA REAL MADRID HUKO DUBAI, EL SHAARAWY ADAI HANA MPANGO WA KUONDOKA MILAN.

MSHAMBULIAJI nyota wa AC Milan, Stephan El Shaarawy amesisitiza hana mpango wowote wa kuondoka katika timu hiyo na badala yake amepania kuipa mafanikio katika mwaka unaokuja. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 22 amekuwa akisumbuliwa na majeruhi katika miezi 12 iliyopita lakini sasa anaonekana kurejea katika kiwango chake tena baada ya kufunga mabao mawili katika ushindi wa mabao 4-2 waliopata dhidi ya Real Madrid jana. Wakati dirisha dogo la usajili likitarajiwa kufunguliwa kesho, El Shaarawy alikuwa akihusishwa na tetesi za kuondoka San Siro lakini mwenyewe sasa amepania amepania kufurahia mwaka ujao akiwa na timu hiyo. Nyota huyo aliwaambia wanahabari huko Dubai ulipofanyika mchezo wao dhidi ya Madrid kuwa hana mpango na hajafikiria kuondoka Milan kwasasa.

No comments:

Post a Comment