Wednesday, December 31, 2014

RAIS WA ATLETICO ADAI SIMEONE NDIO ALIOMBA TORRES ASAJILIWE.

RAIS wa klabu ya Atletico Madrid, Enrique Cerezo amedai kuwa wamemsajili tena Fernando Torres kwa maombi kutoka kwa meneja wa timu hiyo Diego Simeone. Nyota huyo wa kimataifa wa Hispania amekubalia kupelekwa kwa mkopo kwa mabingwa hao wa Hispania baada ya kusajili na AC Milan kwa mkataba wa moja kwa moja kutoka Chelsea. Cerezo anadai kuwa mazungumzo na mshambuliaji huyo yalianza baada ya Simeone kuomba asajiliwe jambo ambalo ni nadra sana kwake. Rais huyo amesema Simeone huwa hana tabia ya kuomba kuomba lakini kwa suala la Torres aliufuata uongozi na kueleza nia yake jambo ambalo wamemtimizia.

No comments:

Post a Comment