Wednesday, December 31, 2014

BALE HAUZWI NG'O - PEREZ.

RAIS wa klabu ya Real Madrid, Florentino Perez amedai kuwa Gareth Bale hawezi kuondoka katika klabu hiyo. Nyota huyo wa kimataifa wa Wales mwenye umri wa miaka 25 ambaye alijiunga na Madrid akitokea tottenham Hotspurs kwa kitita cha paundi milioni 85 mwaka 2013, amekuwa akihusishwa na taarifa za kurejea nchini Uingereza katika klabu ya Manchester United. Akihojiwa Perez amesema hawajapata ofa yeyote kutoka kwa United au klabu yeyote kwa ajili ya Bale. Rais huyo aliendelea kudai kuwa kama anavyofikiria Madrid bila Cristiano Ronaldo ndio anavyofikiria na kwa Bale pia hivyo hadhani kama anaweza kuondoka.

No comments:

Post a Comment