Tuesday, January 27, 2015

VAN PERSIE ADAI HAJUI HATMA YAKE UNITED.

MSHAMBULIAJI wa Manchester United Robin van Persie amekiri hajui kama atapewa ofa ya mkataba mpya wakati ule wa sasa utakapomalizika mwaka 2016. Akihojiwa nyota huyo wa wa kimataifa wa Uholanzi mwenye umri wa miaka 31, amesema hilo sio suala lake kujua kwani anachofahamu kwasasa atakuwepo Old Trafford kwa miezi 18. Van Persie amesema baada ya kumaliza makataba wake hajui kitakaochoendelea baada ya hapo kwani anaweza kuwepo au kuondoka kwenda kwingine. Nyota huyo pia hadhani kama amefunga mabao ya kutosha toka kuanza kwa msimu huu hivyo amepania kuongeza bidii na kuhakikisha anafunga mabao mengi zaidi ili kuisadia timu yake. Van Persie mpaka sasa amefunga mabao nane katika mechi 21 za mashindano yote alizocheza msimu huu na kumaanisha kuwa itakuwa ngumu kufikia rekodi yake ya mabao 18 katika mechi 30 alizocheza katika msimu wake wa kwanza akitokea Arsenal mwaka 2012.

No comments:

Post a Comment