Tuesday, January 27, 2015

NEYMAR ADAI HAWEZI KUMPA USHAURI SUAREZ.

MSHAMBULIAJI wa Barcelona, Neymar anafikiri hana nafasi ya kumpa ushauri Luis Suarez kufuatia mwanzo mgumu katika maisha yake mapya Camp Nou. Nyota huyo wa kimataifa wa Uruguay amekuwa akipambana kurejea katika kiwango chake toka atue Barcelona akitokea Liverpool mwanzoni mwa msimu huu na kupelekea kuachwa katika kikosi cha kwanza katika mchezo wa La Liga mwishoni mwa wiki dhidi ya Elche. Suarez toka atue Camp Nou amezifumania nyavu mara mbili pekee katika mechi 11 alizocheza. Neymar ambaye alipitia wakati kama huo katika msimu wake wa kwanza Barcelona wa 2013-2014, haamini kama yeye ni mtu sahihi wa kumpa ushauri mchezaji mwenzake huyo kukabiliana na hali hiyo. Akihojiwa Neymar amesema suala hilo litakuwa gumu kwake kwakuwa mchezaji huyo kwanza amemzidi umri na pia ana uzoefu mkubwa kuliko yeye hivyo anadhani nyota huyo anapaswa kumpa ushauri yeye.

No comments:

Post a Comment