Tuesday, January 27, 2015

MWENYEKITI WA BAYERN ADAI GUARDIOLA NI ZAIDI YA WAJERUMANI WENYEWE.

MWENYEKITI wa klabu ya Bayern Munich, Karl-Heinz Rummenigge amepongeza kazi nzuri inayofanywa na Pep Guardiola na kutani kuwa kocha huyo wa zamani wa Barcelona anafanana na Wajerumani kuliko Wajerumani wenyewe. Rummenigge amesema kutokana na bidii ya kazi aliyokuwa nayo Guardiola anapaswa kuwa mfano wa kuigwa kwa watu wote. Mwenyekiti huyo aliendelea kudai kuwa wakati wachezaji wote wamerejea nyumbani na kupumzika katika masofa yao, Guardiola yeye huendelea na kazi akipanga mikakati kwa ajili ya mchezo ujao. Kuhusu tetesi za Guardiola kuondoka na kurejea Barcelona, Rummenigge alipuuza taarifa hizo na kudai kuwa kocha huyo ataendelea kuinoa Bayern hata katika msimu ujao wa Bundesliga.

No comments:

Post a Comment