Tuesday, January 20, 2015

ZIDANE AMPASHA POGBA KUWA WACHEZAJI BORA WOTE LAZIMA WAPITIE MADRID.

NGULI wa soka wa zamani wa Ufaransa, Zinedine Zidane amesema wachezaji bora siku zote kujiunga na Real Madrid baada ya kuhojiwa kuhusu nia yao ya kutaka kumsajili nyota Juventus Paul Pogba. Mkurugenzi wa Juventus Giuseppe Marotta amekiri Jana kuwa klabu hiyo inaweza kushindwa kumzuia kiungo huyo mwenye umri wa miaka 21 kwasababu ya mshahara anaoahidiwa na vilabu tajiri barani Ulaya. Marotta pia amebainisha kuwa meneja wa Madrid Carlo Ancelotti tayari ameshamfuata kuhusiana na suala la kiungo huyo wa kimataifa wa Ufaransa. Zidane ambaye kwasasa anakinoa kikosi B cha Madrid amesema hajawahi kujaribu kumshawishi Pogba kujiunga na timu hiyo kwani hafahamiani naye kwa karibu. Lakini Zidane aliendelea kudai kuwa siku zote wachezaji bora lazima waende Real Madrid.

No comments:

Post a Comment