Wednesday, February 18, 2015

RAIS WA PALERMO AITAKA JUVENTUS KUTOA EURO MILIONI 25 KAMA WATAMUHITAJI NYOTA WAKE VAZQUEZ.

RAIS wa klabu ya Palermo Maurizio Zamparini amesema Franco Vazquez anaweza kuigharimu Juventus euro milioni 25 lakini amekanusha kufanyika mazungumzo yeyote juu ya kumuuza kiungo huyo. Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 23 amekuwa akizivutia vilabu kadhaa vya Serie A kutokana na kiwango bora alichokionysha katika msimu wa 2014-2015 huku Napoli nao wakitajwa kumuwinda. Pamoja na Palermo kukanusha kufanya mazungumzo yeyote kuhusu kiungo huyo lakini inaonekana atakayekuja fungu kubwa anaweza kuishawishi timu hiyo kumuuza. Zamparini amesema hakuna klabu yeyote tuliyofanya nao mazungumzo hivyo bado ataendelea kuwa mchezaji wao labda klabu ije na kitita cha paundi milioni 25 ndio tunaweza kufikiria kumuuza. Vazquez bado ana mkataba wa kuitumikia Palermo unaomalizika Juni mwaka 2019.

No comments:

Post a Comment