Monday, March 2, 2015

HENRY AIPIGIA CHAPUO CHELSEA KUPATA MATAJI ZAIDI.

MSHAMBULIAJI wa zamani wa klabu ya Arsenal, Thierry Henry anaamini Chelsea wana uwezo wa kuongeza mataji zaidi msimu huu baada ya kunyakuwa taji la Kombe la Ligi jana. Chelsea jana walifanikiwa kuichapa Tottenham Hotspurs kwa mabao 2-0 katika fainali iliyofanyika katika Uwanja wa Wembley. Henry ambaye kwasasa anafanya kazi kama mchambuzi wa soka amesema anadhani Chelsea wanaweza kuongeza mataji zaidi likiwemo la Ligi Kuu na Ligi ya Mabingwa Ulaya. Henry aliendelea kudai kuwa wana ubora ambao unahitajika kufanya hivyo ndio maana haoni sababu ya kushindwa kufikia malengo hayo.

No comments:

Post a Comment