Monday, March 2, 2015

ROONEY AMKINGIA KIFUA DI MARIA.

NAHODHA wa Manchester United, Wayne Rooney amesema Angel Di Maria atarejea katika kiwango chake pamoja na hivi sasa kuonekana kuwa chini ya kiwango. Baada ya kuanza vyema alipotua Old Trafford, Di Maria ambaye alisajiliwa kwa kitita cha paundi milioni 59.7 kutoka Real Madrid hivi karibuni ameshindwa kuonyesha cheche zake kama alivyozoeleka. Rooney mwenye umri wa miaka 29 amesema Di Maria ni mchezaji bora na hakuna mchezaji anayepoteza kiwango kwa usiku mmoja. Rooney aliendelea kudai kuwa ana uhakika kuwa Di Maria atarejea katika kiwango chake na kuendelea kuifanyia mazuri timu hiyo.

No comments:

Post a Comment