Monday, March 2, 2015

MOURINHO ATAKA MATAJI ZAIDI CHELSEA.

MENEJA wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amedhamiria kutafuta mataji zaidi baada ya kunyakuwa taji la Kombe la Ligi jana ikiwa ni la kwanza kwa kocha huyo toka achukue mikoba ya kuinoa timu hiyo kwa mara ya pili. Mabao yaliyofungwa na Joh Terry na linguine la kujifunga la Kyle Walker yalitosha kuipa ushindi wa mabaop 2-0 Chelsea dhidi ya Tottenham Hotspurs katika mchezo wa fainali uliofanyika katika Uwanja wa Wembley. 
Taji hilo linakuwa la 21 kwa Mourinho toka aanze kufundisha soka. Akihojiwa Mourinho amesema anajiona kama mtoto aliyeshinda kwa mara ya kwanza kwani mara zote imekuwa ngumu kwake kuishi bila mataji. Mourinho ambaye kwa mara ya kwanza amewahi kuinoa Chelsea mwaka 2004 hadi 2007 kabla ya kurejea tena mwaka 2013, hilo linakuwa taji lake la saba akiwa na timu hiyo.

No comments:

Post a Comment