Saturday, February 28, 2015

RODGERS AWAKINGIA KIFUA WACHEZAJI WAKE.

MENEJA wa klabu ya Liverpool, Brendan Rodgers amedai kuwa kikosi chake sio cha kulaumiwa kufuatia kutolewa katika michuano ya Europa League. Liverpool inakabiliwa na mchezo mgumu Jumapili hii dhidi ya Manchester City na Rodgers anataka wachezaji wake kusahau kutolewa huko na kuzingatia mchezo huo. Rodgers amesema anajivunia kikosi chake na jinsi wanavyokabiliana na hali hiyo kwani itawasaidia katika siku zijazo. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa jambo muhimu hivi sasa ni kuhakikisha wanakamata nafasi nne za juu ili waweze kufuzu michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao.

No comments:

Post a Comment