Saturday, February 28, 2015

PARMA YAAHIRISHA MECHI YAO YA SERIE A BAADA YA WACHEZAJI KUTISHIA KUGOMA KWA KUTOLIPWA MISHAHARA YAO.

KLABU ya Parma imelazimika kusogeza mbele mchezo wao wa Seria A dhidi ya Genoa uliokuwa uchezwe Jumapili hii baada ya ya wachezaji kutishia kugoma kutokana na kutolipwa mishahara. Wachezaji wa klabu hiyo ambayo inakabiliwa na matatizo ya kifedha, hawajalipwa toka msimu umeanza huku pia kukiwa na deni la paundi milioni 145. Mwishoni mwa wiki iliyopita mchezo wao dhidi ya Udinese ulilazimika kusitishwa kwasababu maofisa wa klabu kushindwa kulipa fedha walizokuwa wakidaiwa. Shirikisho la Soka la Italia-FIGC limeionya Parma dhidi ya kuahirisha mechi zake katika siku za usoni.

No comments:

Post a Comment