Saturday, February 28, 2015

HENRY AKITAMANI KIBARUA CHA WENGER.

MCHEZAJI nyota wa zamani wa klabu ya Arsenal, Thierry Henry amedai kuwa ndoto yake ni kumrithi kocha wa sasa Arsene Wenger. Mapema mwezi huu Henry ambaye ndio anaongoza kwa kufunga mabao mengi katika klabu hiyo alipewa ofa ya kuanza kufundisha soka katika shule ya soka ya timu hiyo. Akihojiwa Henry raia wa Ufaransa amekiri kuwa anatamani siku moja aweze kurithi mikoba ya Wenger kama kocha wa Arsenal. Wakati akiichezea Arsenal Henry amefanikiwa kufunga mabao 228 idadi ambayo hakuna mshambuliaji yeyote wa timu amewahi kuifikia mpaka sasa.

No comments:

Post a Comment