Saturday, February 28, 2015

VAN GAAL ADAI UNITED INAHITAJI MSHAMBULIAJI MWENYE UWEZO KUFUNGA MABAO 20 KWA MSIMU.

MENEJA wa klabu ya Manchester United, Louis van Gaal amesema kikosi chake kinakosa mshambuliaji mwenye uwezo wa kufunga mabao 20 kwa msimu. United kwasasa wanashika nafasi ya nne katika msimamo wa Ligi Kuu wakiwa nyuma ya vinara Chelsea kwa alama nne huku wakikabiliwa na upinzani mkali wa kupata nafasi ya kufuzu michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao. Robin van Persie ndiye anaongoza kwa kufunga mabao United akiwa amefunga mabao 10 msimu huu lakini sasa anakabiliwa na kipindi kirefu cha kukaa nje kutokana na majeruhi yanayomsumbua. Radamel Falcao amekuwa akipambana kujaribu kuzoea soka la Uingereza huku Wayne Rooney mara nyingi akiwa anapangwa katika nafasi ya kiungo. Akihojiwa Van Gaal alikiri kuwa anakosa aina ya mshambuliaji mwenye uwezo wa kufunga mabao zaidi ya 20 kwa msimu jambo limekuwa tatizo kwa kikosi chake msimu huu. Van Gaal amesema wachezaji karibu wote katika kikosi chake wamekuwa wakijaribu kuzoea mazingira mapya na mbinu mpya hivyo anadhani wanaweza kufikia malengo yao mpaka mwishoni mwa msimu.

No comments:

Post a Comment